KABLA YA KUWEKEZA KWENYE BIASHARA YAKO ANZA NA WEWE MWENYEWE

1

Ni shauku ya kila mtu kuwa na biashara yenye uwekezaji mkubwa na miundo mbinu mikubwa lakini kabla ya kuwekeza kwenye eneo lolote anza kuwekeza kwako mwenyewe.

2

Kama unatamani kuwekeza katika kilimo biashara wekeza muda wa kijifunza kwenye hili eneo ujue kilimo biashara kikoje, kinaendeshwaje, kina changamoto gani.

3

Tafuta vikundi vya wakulima na taasisi ambazo zinawajengea uwezo wakulima jiunge nao halafu shiriki kwenye mafunzo mbalimbali hususani yale ya shamba darasa usiache.

4

Tafuta wakulima wanaofanya shughuli hiyo na wafanyabiashara jifunze kwao kwasababu wao wanaujuzi kutoka kwenye wanja wa kilimo hivyo maaarifa yao sio nadharia.

5

Mara nyingi ukiwasikiliza watu ambao wamefanikiwa katika biashara fulani utasikia wakielezea mazuri,

6

faida wanayopata na mafanikio waliyonayo kama unatamani kufanya vizuri kwenye biashara jifunze hao watu walifanikiwaje, walitumia mbinu gani, wanapata changamoto gani na je wanakabiliana nayo vipi?

7